UNICEF yatangaza ombi la misaada ya kuhudumia Chad
Shirika la UM juu ya Maendeleo ya Watoto (UNICEF) wiki hii limetangaza ombi maalumu lenye kuwahimiza wahisani wa kimataifa kufadhilia msaada wa dharura wa dola milioni 9 kukidhia mahitaji ya mamia elfu ya wahamiaji waliopo kwenye maeneo ya mashariki na kusini ya Chad.