KM ahimiza kuwepo ushikiriano wa kimataifa kuisaidia Afrika kuepukana na umasikini
KM Kofi Annan Alkhamisi alitoa risala maalumu mjini Addis Ababa, Ethiopia mbele ya wajumbe waliohudhuria Mkutano juu ya Maendeleo ya Afrika, ambapo alionya ya kwamba pindi wahisani wa kimataifa watashindwa kushirikiana na UM pamoja na mataifa yanayoendelea kuisaidia Afrika kuimarisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii kuna hatari ya bara hilo kunyimwa huduma za kuimarisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii na, hatimaye, hata kunyimwa fursa ya kuyafikia, kwa wakati, yale Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs).