Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR kuhudumia maelfu ya wahamiaji wa Usomali walioathiriwa na mafuriko nchini Kenya

UNHCR kuhudumia maelfu ya wahamiaji wa Usomali walioathiriwa na mafuriko nchini Kenya

Shirika la UM juu ya Wahamiaji (UNHCR) limeripotiwa kushiriki hivi sasa kwenye shughuli kuhudumia misaada ya kihali kwa maelfu ya Wasomali walioathirika na maafa ya mvua kali zilizojiri karibuni katika eneo la kaskazini-mashariki ya Kenya, hususan katika zile kambi za wahamiaji za jimbo la Dadaab. Kwa mujibu wa UNHCR mvua hizo zilizusha mafuriko yalioeneza uharibifu mkubwa katika sehemu hiyo ya nchi.~