Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM bado anasubiri idhini ya Sudan juu ya vikosi vya mseto vya UM/AU kwa Darfur

KM bado anasubiri idhini ya Sudan juu ya vikosi vya mseto vya UM/AU kwa Darfur

KM Kofi Annan alikuwa na mashauriano na Baraza la Usalama wiki hii kuhusu hali katika Darfur,Sudan. Baada ya mkutano wake huo na Baraza la Usalama aliwaambia waandishi habari wa kimataifa waliopo Makao Makuu kwamba Serekali ya Sudan bado haijamtumia jawabu yao ya kuidhinisha maafikiano ya kimsingi, waliokubaliana pamoja wiki iliopita, ya kupeleka vikosi vya mseto vya UM na AU katika Darfur ambayo yanahitajika kidharura kukomesha uhasama na maafa yaliofumka na kutanda kwenye eneo hilo, na kuathiri vibaya maisha ya malaki ya raia.