Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vikosi vya MONUC kushiriki kwenye doria ya kuulinda mji mkuu wa Congo-DRC

Vikosi vya MONUC kushiriki kwenye doria ya kuulinda mji mkuu wa Congo-DRC

Wanajeshi wa Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, yaani Shirka la MONUC wameanzisha, wiki hii, doria yenye mada isemayo “Kinshasa, mji usio silaha”, kwa makusudio ya kuzuia vikundi vyenye kuchukua silaha kutoaranda randa ovyo na kuzusha fujo na vurugu, hususan katika kipindi ambacho taifa linajiandaa kufanya duru ya pili ya uchaguzi wa raisi mwisho wa Oktoba. Vikosi vya MONUC vinashirikiana kwenye doria hii maalumu na majeshi ya taifa ya Congo-DRC pamoja na vikosi vya polisi vya kutoka Umoja wa Ulaya.