Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mikakati ya kupambana na UKIMWI Inahitaji Kubadilishwa

Mikakati ya kupambana na UKIMWI Inahitaji Kubadilishwa

Wanasayansi, wakuu wa mashirika ya kimataifa, wawakilishi wa kiserekali na pia wale kutoka mashirika yasio ya kiserekali waliohudhuria mkutano wa kihistoria juu ya UKIMWI mjini Toronto, Kanada katika mwezi Agosti walitoa mwito uliopendekeza ile mikakati ya kupambana na janga la virusi vya UKIMWI (VVU) na UKIMWI wenyewe ibadilishwe. A. Aboud kutoka Redio ya UM alihudhuria mkutano huo wa Toronto na alitayarisha ripoti maalumu juu ya pendekezo hilo. Kwa taarifa kamili sikiliza idhaa ya mtandao ya Umoja wa Mataifa.~