Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mukhtasari unaongaza wiki ya kwanza ya mjadala wa wawakilishi wote katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa

Mukhtasari unaongaza wiki ya kwanza ya mjadala wa wawakilishi wote katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa

Mjadala wa kila mwaka wa wawakilishi wote kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ulifunguliwa rasmi hapo Ijumanne, tarehe 19 Septemba (2006) na Sheikha Haya Rashed Al Khalifa wa Bahrain. Sheikha Haya katika hotuba yake ya ufunguzi aliwahimiza viongozi wa kimataifa waliokusanyika kwenye Makao Makuu kulenga zaidi juhudi zao katika kutekeleza kwa vitendo ahadi zao ili kusaidia kupunguza ufukara na kuboresha maisha ya umma wa kimataifa, kwa ujumla. ~