Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM kutoa ripoti juu ya udhibiti wa mirando ya magaidi duniani

UM kutoa ripoti juu ya udhibiti wa mirando ya magaidi duniani

Ripoti mpya ya UM kuhusu suala la ugaidi duniani imepongeza ushirikiano uliojiri karibuni ambapo Mataifa Wanachama yameanza kuonesha “umoja wa kimawazo” kwenye zile juhudi za kuvinyima vikundi vya kigaidi ulimwenguni fursa ya kuvuka ile mipaka iliyokosa ulinzi imara na ambapo nyaraka bandia hutumiwa bila pingamizi.