Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sudan kupata huduma za afya kutoka serikali ya Japan

Sudan kupata huduma za afya kutoka serikali ya Japan

Akina mama na watoto wa kaskazini mwa Sudan watafarijika hivi sasa kwa kuweza kupata machanjo muhimu ya kuokoa maisha na madawa ya malaria pamoja na huduma za afya kutokana na msaada kutoka serekali ya Japan wa dola milioni 4.5 ulokabidhiwa UNICEF. Shirika la watoto linaeleza kua msaada huo utasaidia kuimarisha afya ya kiasi ya watu milioni 3 na nusu.