Ripoti ya KM kuhusu mzozo nchini Uganda Kaskazini.
Ripoti ya KM iliyowasilishwa karibuni kuhusu mzozo wa Uganda ya Kaskazini imesisitiza ya kuwa licha ya Serekali za mataifa jirani kujaaliwa uwezo na dhamana ya kukabiliana na utenguzi wa haki za kiutu unaoendelezwa na kundi la waasi la LRA dhidi ya raia, kwa wao kuweza kulidhibiti tatizo hilo kithabiti na kusawazisha usalama wa eneo, watahitajia vile vile msaada na ujuzi wa UM.~~