Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwakilishi wa KM kwa Usomali apendekeza ujumbe wa kurudisha amani

Mwakilishi wa KM kwa Usomali apendekeza ujumbe wa kurudisha amani

Mwakilishi Maalumu wa KM kwa Usomali, Francois Lonseny Fall wiki hii amemtumia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kundi la Mahakama za Kiislamu mjini Mogadishu barua inawayohimiza kupeleka wawakilishi wao kwenye duru ya pili ya mazungumzo ya kurudisha amani katika Somalia yaliyoandaliwa kufanyika Khartoum, Sudan kati yao na viongozi wa Serekali ya Mpito ya Usomali.