Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM yaahidi kuongeza misaada ya kiutu Lebanon

UM yaahidi kuongeza misaada ya kiutu Lebanon

Ilivyokuwa matatizo ya kiutu bado yanaendelea kukithiri katika mazingira ya vita katika Lebanon ya kusini UM umeripoti ya kuwa utalazimika kupeleka misafara ziada ya misaada ya kihali katika miji ya Jezzine na Sidon ili kukidhia mahitaji ya kunusuru maisha kwa umma waathiriwa wa maeneo haya. Hatua hii imechukuliwa baada ya msafara wa UM kufanikiwa Ijumanne kupeleka katika mji wa bandari wa Tyre shehena za chakula na mahitaji mengineyo ya kiutu.