Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wanajeshi waangalizi wanne wa UM Kuuwawa Lebanon

Wanajeshi waangalizi wanne wa UM Kuuwawa Lebanon

Naibu KM wa Idara ya UM juu ya Operesheni za Amani Duniani, Jane Holl Lute aliripoti mbele ya Baraza la Usalama wiki hii kwamba wanajeshi waangalizi wanne wa ulinzi wa amani wasiochukua silaha kutoka Austria, Kanada, Finland ~na Uchina, waliuawa Ijumanne kwa mizinga ya majeshi ya Israel ambayo tuliarifiwa ililengwa moja kwa moja, sawia, kwenye kituo cha uangalizi cha UM karibu na mji wa Khiam, Lebanon ya kusini.