Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Idadi ya wanaoingia jengo la UN New York yapunguzwa kwa asilimia 60 ili kupambana na COVID-19
Wakati maambukizi mapya ya virusi vya Corona au COVID-19 yakiendelea kuongezeka katika nchi nyingi duniani na idadi ya waliofariki kutokana na virusi hivyo ikiongezeka kila uchao, Umoja wa Mataifa nao umechukua hatua kudhibiti maambukizi kwa kupunguza idadi ya wafanyakazi wanaofika kazini kila siku kwa asilimia 60. Hii ni kwa kuzingatia kuwa tayari visa vimeripotiwa katika miji kadhaa ikiwemo New York, Marekani ambako ndiko makao makuu ya chombo hicho.
11 Machi 2020
UN yachukua hatua madhubiti kudhibiti COVID 19. Mataifa lazima yafundishe watoto wa kiasili na wale wa jamii za wachache kwa lugha yao wenyewe asema mtaalam wa UN. Usiache mila na deturi zikazima ndoto zako ashauri Mama mwendesha Bodaboda Palagie Gerald.
COVID-19: Idadi ya wanaoingia jengo la UN New York yapunguzwa kwa asilimia 60 wakiwemo wafanyakazi
Wakati maambukizi mapya ya virusi vya Corona au COVID-19 yakiendelea kuongezeka katika nchi nyingi duniani na idadi ya waliofariki kutokana na virusi hivyo ikiongezeka kila uchao, Umoja wa Mataifa nao umechukua hatua kudhibiti maambukizi kwa kupunguza idadi ya wafanyakazi wanaofika kazini kila siku kwa asilimia 60. Hii ni kwa kuzingatia kuwa tayari visa vimeripotiwa katika miji kadhaa ikiwemo New York, Marekani ambako ndiko makao makuu ya chombo hicho.
Chonde chonde virusi vya Corona visilete rabsha kwenye elimu - UNESCO
Idadi ya maambukizi mapya ya virusi vya Corona ikiongezeka duniani sambamba na watu waliofariki dunia, Umoja wa Mataifa umetaka hatua zichukuliwe ili kuepusha janga hilo kusambaratisha elimu wakati huu ambapo hatua zinazochukuliwa kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa huo ni pamoja na kufunga shule na vyuo vikuu.
Ukuaji wa uchumi duniani watishiwa na COVID-19:UNCTAD
Mgogoro wa kimataifa wa kiafya uliosababishwa na janga la virusi vya corona au COVID-19 unaweza kuwa na athari kubwa za kiuchumi, na kusababisha upungufu wa dola bilioni 2, 000, pamoja na dola bilioni 200 kwa nchi zinazoendelea, kulingana na moja ya matarajio mabaya yaliyotolewa leo Jumatatu kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD huko Geneva Uswis.
Umoja wa Mataifa waeleza CSW64 ni fursa ya kuchagiza kasi ya kufikia usawa wa kijinsia
Kikao cha 64 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW64 kimeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani , ingawa hakitofanyika kwa wiki mbili kama ilivyo ada.
09 MACHI 2020
CSW64 ni fursa ya kuchagiza kasi ya kufikia usawa wa kijinsia, umesema Umoja wa Mataifa. Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, baadhi ya wanawake waliopona ugonjwa wa Ebola wametoa shukrani zao kwa mamlaka. Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema idadi ya watoto waliovuka pori la Darien linalotenganisha Colombia na Amerika ya Kati mwaka 2019 imeongezeka zaidi ya mara saba.
Visa vya COVID-19, Jumamosi hii vimefikia 100,000:WHO
Idadi ya visa vya Corona, COVID19 vimepita laki moja kote duniani kwa mujibu wa taarifa ya shirika la afya duniani, WHO iliyotolewa Jumamosi.
Virusi vya Corona vyatikisa uchumi wa dunia, uzalishaji China wasinyaa- UNCTAD
Kamati ya maendeleo ya biashara ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD, imesema virusi vya Corona au COVID-19, vimesababisha uzalishaji nchini China kusinyaa kwa asilimia 2 katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
Virusi vya Corona vyasababisha kuahirishwa kwa mkutano wa 64 wa CSW
Virusi vya Corona au COVID-19 vimeendelea kuathiri shughuli a kiuchumi, kijamii na kisiasa duniani na athari hasi za hivi karibuni zaidi ni kuahirishwa kwa mkutano wa 64 wa Kamisheni ya hali ya wanawake duniani, CSW uliokuwa ufanyike kwa wiki mbili hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kuanzia tarehe 9 hadi 20 mwezi huu wa Machi.