Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

05 APRILI 2021

Ugonjwa wa Corona au COVID-19 ulizua zahma kubwa duniani ulipoibuka mwaka jana na kuleta sintofahamu. Hali hiyo bado haijaisha hadi sasa ambapo ni mwaka mmoja umeshapita na watu zaidi ya milioni 128 wameugua duniani kote hadi sasa na kati yao hao zaidi ya milioni 2.8 wamefariki dunia. Bado mazuio ya safari yamewekwa katika baadhi ya nchi na masharti ya kujikinga kwa kuvaa barakoa, kuepuka michangamano na kutumia vitakasa mikono zinazingatiwa. Hata hivyo chanjo imepatikana na inaleta nuru.

Sauti
10'51"
UNICEF ikifikisha shehena ya chanjo dhidi ya COVID-19 nchini Msumbiji
UNICEF

Mwaka mmoja wa janga la COVID-19 kuna nuru gizani:Guterres

Baada ya miezi 12 ya ulimwengu kukabiliwa na "tsunami ya mateso", kuwasili kwa chanjo dhidi ya janga la corona au COVID-19 inashiria nuru fulani baada ya kiza totoro" amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa leo Alhamisi,ikiwa ni maadhimisho yam waka mmoja tangu shirika la afya la Umoja wa Mataifa (WHO) ) kutangaza rasmi kuwa janga hilo ni la kimataifa.

UN/ John Kibego

Vijana wa kike wahimizwa kupigania haki za kumiliki ardhi Uganda.

Wiki hii dunia ikiwa imeadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake duniani ambapo sehemu mbalimbali wanawake waliitumia kuonesha kero zao na kutiana moyo. Nchini Uganda, wanawake katika wilaya ya Buliisa wameandamana hadi Makao Makuu ya wilaya hiyo kuwasilisha malalamiko yao wakiitaka serikali ishughulikie changamoto yao ya kunyimwa haki ya kumiliki ardhi.

Sauti
3'51"
Watoto katika shule nchini Haiti wakipata chakula kama sehemu ya mpango wa mlo shuleni wa WFP.
UN Photo/Leonora Baumann

Theluthi 2 ya mwaka wa masomo duniani imepotea sababu ya COVID-19:UNESCO

Ikiwa ni mwaka mmoja sasa tangu kuzuka kwa janga la corona au COVID-19, Zaidi ya wanafunzi milioni 800 ambao ni zaidi ya nusu ya wanafunzi wote duniani bado wanakabiliwa changamoto kubwa ya kuvurugwa kwa elimu yao, kuanzia kufungwa kwa shule katika nchi 31 hadi kupunguzwa au kusoma kwa muda mfupi katika nchi zingine 48 kwa mujibu wa takwimu mpya zilizotolewa leo kupitia ramani ya ufuatiliaji ya shirika la Umoja wa Mataifa la elimu na utamaduni UNESCO.

06 JANUARI 2021

Katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea

- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa atoa wito wa kuhakikisha mizozo inasitishwa na mizizi yake kukatwa kwa lengo la kudumisha amani na kufikia ajenda ya maendeleo ya 2030 hususan brani Afrika.

-Walinda amani kutoka Burundi, Bangladesh na Cameroon waliopoteza maisha Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR wakati wa Krisimasi waagwa na kusafirishwa makwao kwa maziko

Sauti
11'34"