Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Sven Torfinn/WHO 2016

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO yazindua mkakati kutokomeza malaria katika nchi 25 ifikapo 2025 

Katika kuelekea  siku ya malaria duniani, inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Aprili,  shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limepongeza idadi kubwa ya nchi zinazokaribia na kufikia, utokomezajhji kabisa wa malaria. Taarifa ya Jason Nyakundi inaeleza kwa kina.

Mpango mpya uliozinduliwana shirika hilo unakusudia kusitisha maambukizi ya ugonjwa huo katika nchi 25 zaidi ifikapo mwaka 2025. 

Ripoti ya WHO inasema kati ya nchi 87 zilizo na malaria, 46 ziliripoti chini ya visa 10,000 vya ugonjwa huo mwaka 2019 ikilinganishwa na nchi 26 mwaka 2000.  

Sauti
3'36"