Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

UNICEF ikifikisha shehena ya chanjo dhidi ya COVID-19 nchini Msumbiji
UNICEF

Mwaka mmoja wa janga la COVID-19 kuna nuru gizani:Guterres

Baada ya miezi 12 ya ulimwengu kukabiliwa na "tsunami ya mateso", kuwasili kwa chanjo dhidi ya janga la corona au COVID-19 inashiria nuru fulani baada ya kiza totoro" amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa leo Alhamisi,ikiwa ni maadhimisho yam waka mmoja tangu shirika la afya la Umoja wa Mataifa (WHO) ) kutangaza rasmi kuwa janga hilo ni la kimataifa.