Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Wanafunzi waliporejea darasani katika shule ya msingi San Pedro Kusini Magharibi mwa Côte d'Ivoire.
© UNICEF/Frank Dejo

Watoto katika nchi maskini wamepoteza miezi minne ya masomo tangu kuanza kwa janga la COVID-19-Ripoti 

Watoto wa shule katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati chini, tayari wamepoteza takribani miezi minne ya masomo tangu kuanza kwa janga la virusi vya corona ikilinganishwa na wiki sita za upotezaji masomo katika nchi zenye kipato cha juu. Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa hii leo mjini New York na Washington Marekani pamoja na Paris Ufaransa na mashirika ya Umoja wa Mataifa lile la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO na la kuhudumia watoto UNICEF kwa kushirikiana na  Benki ya Dunia. 

Sauti
2'57"