Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Makazi kwa wote ndio chachu ya mustakbali bora mijini:UN-HABITAT
Kuwa makazi bora hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote ni suala la uhai na kifo hasa janga la corona likiendelea kusambaa duniani na watu wakitakiwa kusalia majumbani, lakini hatua hiyo haiwezekani hasa kwa wale ambao hawana wanapopaita nyumbani limesema shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT.
Kutoka darasani hadi shambani, mwalimu kutoka Uganda azungumza
Leo ikiwa ni siku ya walimu duniani, ambayo mwaka huu inaadhimishwa kukiwa na changamoto kubwa kwa walimu na wanafunzi kufuatia janga la corona au COVID-19, huku Umoja wa Mataifa ukisema takriban wanafunzi bilioni 1.6 ambao ni zaidi ya wanafunzi wote duniani waliojiandikisha shule wameathiriwa na kufungwa kwa shule.
05 Oktoba 2020
COVID-19 yamlazimisha mwalimu kusaka kipato mbadala nchini Uganda. UN-HABITAT yachukua hatua kupambana na COVID-19 hata kwa wasio na makazi Kenya. Elimu ya IFAD yawasaidia wanawake wa Kontagora, Nigeria kuwa mamilionea.
COVID-19 yamlazimisha mwalimu kusaka kipato mbadala nchini Uganda
Leo ikiwa ni siku ya walimu duniani, ambayo mwaka huu inaadhimishwa kukiwa na changamoto kubwa kwa walimu na wanafunzi kufuatia janga la corona au COVID-19, huku Umoja wa Mataifa ukisema takriban wanafunzi bilioni 1.6 ambao ni zaidi ya wanafunzi wote duniani waliojiandikisha shule wameathiriwa na kufungwa kwa shule.
UN-HABITAT yachukua hatua kupambana na COVID-19 hata kwa wasio na makazi Kenya
Ikiwa leo ni siku ya makazi duniani, kuwa na makazi bora imeelezwa hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote ni suala la uhai na kifo hasa janga la corona au COVID-19 likiendelea kusambaa duniani na watu wakitakiwa kusalia majumbani, lakini hatua hiyo haiwezekani hasa kwa wale ambao hawana wanapopaita nyumbani limesema shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT.