Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Hakuna nchi hata moja inaweza peke yake kumudu janga kama hili la COVID-19
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya hii leo akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya vdeo iliyorekodiwa kutokana na janga la virusi vya corona kutoruhusiu viongozi wa dunia kukutana New York Marekani kama ilivyo ada ya kila mwaka, ameueleza ulimwengu kuwa ugonjwa wa COVID-19 linapaswa kutoa msukumo mpya, “kwa juhudi zetu za pamoja za kuimarisha ushirikiano wa kimataifa.” Na hakuna nchi ambayo peke yake inaweza kumudu janga kubwa la kiwango cha COVID-19.
Taarifa potofu ziliongeza changamoto katika kukabili Corona
Umoja wa Mataifa na wadau wamezisihi nchi zote duniani kushughulikia kile walichoekelea kuwa ni janga la taarifa ambalo limeibuka kutokana na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, katika ulimwengu wa kawaida na mtandaoni.
UN iko tayari kuyasaidia mataifa yasiyo na bahari, kujikwamua na COVID-19
Mfumo wa umoja wa Mataifa umesema unashikamana na mataifa yanayoendelea yasiyo na bahari ambayo yanakosa fursa muhimu za viunganishi vya biashara na kuyasaidia katika juhudi zao za kujijenga upya pindi janga la corona au COVID-19 litakapokwisha.
Lugha ya ishara lazima ijumuishwe katika kujikwamua na janga la COVID-19
Mwaka huu siku ya kimataifa ya lugha ya ishara inaadhimishwa katikati ya janga la corona au COVID-19, janga ambalo limemkumba kila mtu wakiwemo jamii ya viziwi, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Siri ya Tanzania katika kuidhibiti COVID-19
Wakati hii leo, wakuu wa nchi na wawakilishi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanashiriki mkutano wa ngazi ya juu wa UNGA75 wa kujadili jinsi ya kuepusha upotoshaji wa taarifa na usambazaji wa taarifa potofu wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, Tanzania imetaja siri ya mafanikio yake katika kudhibiti gonjwa hilo mara baada ya kubainika mwezi Machi mwaka huu. Flora Nducha na maelezo zaidi.
Tanzania haikuongozwa na mihemuko ya kisiasa katika kukabili COVID-19 – Balozi Gastorn
Wakati hii leo, wakuu wa nchi na wawakilishi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanashiriki mkutano wa ngazi ya juu wa UNGA75 wa kujadili jinsi ya kuepusha upotoshaji wa taarifa na usambazaji wa taarifa potofu wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, Tanzania imetaja siri ya mafanikio yake katika kudhibiti gonjwa hilo mara baada ya kubainika mwezi Machi mwaka huu.