Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya akihutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA75 kwa njia ya video.
UN Photo/Evan Schneider

Hakuna nchi hata moja inaweza peke yake kumudu janga kama hili la COVID-19

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya hii leo akihutubia mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa njia ya vdeo iliyorekodiwa kutokana na janga la virusi vya corona kutoruhusiu viongozi wa dunia kukutana New York Marekani kama ilivyo ada ya kila mwaka, ameueleza ulimwengu kuwa ugonjwa wa COVID-19 linapaswa kutoa msukumo mpya, “kwa juhudi zetu za pamoja za kuimarisha ushirikiano wa kimataifa.” Na hakuna nchi ambayo peke yake inaweza kumudu janga kubwa la kiwango cha COVID-19. 

UN News/Anold Kayanda

Siri ya Tanzania katika kuidhibiti COVID-19

Wakati hii leo, wakuu wa nchi na wawakilishi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanashiriki mkutano wa ngazi ya juu wa UNGA75 wa kujadili jinsi ya kuepusha upotoshaji wa taarifa na usambazaji wa taarifa potofu wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, Tanzania imetaja siri ya mafanikio yake katika kudhibiti gonjwa hilo mara baada ya kubainika mwezi Machi mwaka huu. Flora Nducha na maelezo zaidi. 

Sauti
1'56"
Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa, Balozi Kennedy Gastorn wakati wa mahojiano na Idhaa ya Umoja wa Mataifa.
UN News/Anold Kayanda

Tanzania haikuongozwa na mihemuko ya kisiasa katika kukabili COVID-19 – Balozi Gastorn

Wakati hii leo, wakuu wa nchi na wawakilishi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanashiriki mkutano wa ngazi ya juu wa UNGA75 wa kujadili jinsi ya kuepusha upotoshaji wa taarifa na usambazaji wa taarifa potofu wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19, Tanzania imetaja siri ya mafanikio yake katika kudhibiti gonjwa hilo mara baada ya kubainika mwezi Machi mwaka huu. 

Sauti
1'56"