Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akifungua tukio la kwanza la Malengo ya maendeleo endelevu SDGs.
UN Photo/Eskinder Debebe)

Tukio la SDGs laadhimishwa kwa mara ya kwanza 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo amefungua tukio la Malengo ya maendeleo endelevu, SDG jijini New York Marekani ambalo litakuwa linafanyika kila mwaka katika miaka hii kumi ya kuelekea kutimiza malengo hayo ifikapo mwaka 2030. Bwana Guterres ameuambia ulimwengu kupitia mkutano hio kuwa tukio hili la kujadili masuala ya malengo endelevu ni fursa kuonesha kuwa kama familia moja ya mataifa iliyoungana, “tuna kila kinachotakiwa ili kutokomeza umaskini na njaa, kudhibiti mabadiliko ya tabianchi, kufikia usawa wa kijinsia na kufanikisha malengo 17 ya kimataifa.”