Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Ushirika wa mataifa ya Kusini-SSC- umetoa mafunzo ya maelekezo kuhusu ulimaji wa mpunga Cote D'ivoire.
©FAO/Wang Jinbiao

Ushirikiano baina ya nchi za kusini umekuwa jawabu wakati huu wa COVID-19

Utashi wa ushirikiano baina ya nchi za kusini au zile zinazoendelea na mshikamano wa dunia bado uko hai ulimwenguni kote wakati huu ambapo tunahaha kukabiliana na janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya ushirikiano wa nchi za kusini hii leo.