Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

© UNICEF/UNI312809// Frank Dejongh

Ripoti yaonesha COVID-19 yaweza futa mafanikio ya kupunguza vifo vya watoto wachanga 

Ripoti mpya iliyotolewa leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa na taasisi zake, imeonesha kuwa mafanikio yaliyopatikana takribani miongo mitatu katika kuepusha vifo vya watoto wachanga yanaweza kufutwa na janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 iwapo hatua madhubuti hazitachukuliwa. 

Ikiwa na makadirio mapya ya vifo vya watoto wachanga, ripoti hiyo inasema kuwa idadi ya vifo imepungua kutoka milioni 12.5 mwaka 1990 hadi vifo milioni 5.2 mwaka wa 2019. 

Sauti
2'8"