Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataif kwa Syria, Geir O.pedersen akizungumza na wanahabari. (PIcha ya maktaba)
UN Photo/Evan Schneider

Natiwa moyo na angalau kuwepo kwa misimamo ya pamoja baina ya pande kinzani Syria- Pedersen 

Wajumbe wa pande kinzani nchini Syria wanaokutana mjini Geneva, Uswisi kwa lengo la kusaka suluhu ya kudumu na kumaliza mzozo wa takribani muongo mmoja nchini mwao, angalau wamekuwa na misimamo inayofanana itakayoweza kusongesha mbele majadiliano, amesema Geir Pedersen, Mjumbe Maalum wa Umoja wa Mataifa kwa mzozo wa Syria.