Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

World Bank/Curt Carnemark

Tanzania tumeshinda tuzo na utalii umerejea– TTB

Wakati janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 likiendelea kusababisha zahma kwingineko duniani na hata kukwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii, nchini Tanzania hali ni tofauti, utalii umerejea na tuzo juu ya kimataifa, kulikoni?  Stella Vuzo wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa, UNIC jijini Dar es salaam, Tanzania amemhoji Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii Tanzania, TTB, Devotha Mdachi.

 

Sauti
6'1"
Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini Tanzania, Christine Musisi akizindua moja ya magari ya wagonjwa ambayo yamebadilishwa kutoka magari ya kawaida kufuatia msaada wa fedha kutoka shirika hilo la UN.
UNDP/Sawiche Wamunza

UNDP yapigia chepuo uimarishaji wa sekta ya utalii Tanzania

Nchini Tanzania, shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP limeshiriki katika uzinduzi wa moja kati ya magari matatu ya magonjwa ambayo yatatumika katika hifadhi ya Taifa na mbuga za wanyama wakati huu ambapo taifa hilo la Afrika Mashariki limefungua tena milango yake kwa watalii wa nje na wa ndani.

Afisa wa mbuga ya taifa nchini Tanzania akipima joto la mtalii kama moja ya kanuni za kudhibiti ugonjwa wa COVID-19.
TTB Video screenshot

Miongozo ya utalii imetuwezesha kushinda tuzo na utalii umerejea Tanzania – TTB

Wakati janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19 likiendelea kusababisha zahma kwingineko duniani na hata kukwamisha shughuli za kiuchumi na kijamii, nchini Tanzania hali ni tofauti na kutokana na kuzingatia kanuni za kulinda wananchi na watalii, shughuli za utalii zimerejea na hata taifa hilo la Afrika Mashariki limepata tuzo ya Mhuri wa kimataifa. 

Sauti
6'1"