Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Mpangilio wa ukaaji na pia ngao za kutenganisha kati ya mtu na mtu vimewekwa ili kuhakikisha umbali kati ya mtu na mtu katika hospitali mjini Bangkok, Thailand
ILO/Alin Sirisaksopit

Wagonjwa wa COVID-19 watafikia milioni 20 wiki hii-WHO 

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa Dkt Tedros Ghebreyesus ameueleza ulimwengu hii leo kuwa, wiki hii idadi ya wagonjwa wa COVID-19 walioathibitishwa itafikia milioni 20 na vifo 750,000 kote duniani  kwa hivyo viongozi wanatakiwa kuchukua hatua na raia wanatakiwa kuzifuata au kuzikumbatia hatua mpya.

10 Agosti 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo na Assumpta Massoi 
- Shirka la Umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) nchini Uganda leo limesema limesikitishwa na kifo cha kwanza kabisa cha mkimbizi kutokana na virusi vya corona au COVID-19 tangu mlipuko huo utangazwe nchini humo mnamo Machi mwaka huu.
-Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaendelea na juhudi za kuokoa maisha Beirut 
- Watafiti wa malaria barani Afrika wameonya kuwa huenda bara hilo likajikuta katika hali ngumu ya kupambaan na ugonjwa wa malaria unaokatili maisha ya maelfu ya watu kila mwaka na
Sauti
11'47"