Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

UN/ John Kibego

COVID-19 Uganda yawa ‘mwiba’ kwa akina mama wanaonyonyesha watoto

Maziwa ya mama bado hayajathibitishwa kuwa na uwezo wa kuambukiza virusi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto," imesema WHO wakati huu ambapo kuna shaka na shuku kuwa yanaweza kusababisha maambukizi.

Wiki ya kimataifa ya unyonyeshaji mtoto maziwa ya mama ikifikia ukingoni hii leo, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, limesema kuwa bado hakuna uthibitisho wowote ya kwamba virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Corona, au COVID-19, vinaweza kuambukizwa kupitia maziwa ya mama.

Sauti
1'56"