Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

UNICEF/Habib Kanobana

Mwalimu aeleza changamoto za kiuchumi na kijamii kutokana na COVID-19, Uganda

Elimu bora kwa wote ni miongoni mwa malengo ya maendeleo endelevu au SDGs, lengo ambalo limeingia mashakani kutokana na mlipuko wa COVID-19 kwani serikali nyingi zimelazimika kufunga taasisi za elimu zote kama njia za kuudhibiti. Tuelekee nchini Uganda ambako John Kibego amezungumza na Mwalimu Charles Okuta, mmoja wa walimu waliochaguliwa kutoa mafunzo kwa njia ya redio katika wilaya ya Bwikwe kwa msaada kutoka shirika la World Vision tawi la Bwikwe.

Sauti
3'14"