Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

05 JUNE 2020

Jaridani la Umoja wa Maitafa leo ikiwa Ijumaa ni mada kwa kina ambapo tutamulika athari za gonjwa la virusi vya Corona katika kulinda wanyama walio hatarini kutoweka.
- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa asema tubadili tabia tulinde mazingira kwani muda unayoyoma
-  Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa leo imesema takribani watu 1,300 ambao ni raia wameuawa katika matukio tofauti nchini DRC. 
- Na shirika la Uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM limesaidia raia 179 wa Mali waliokuwa wamekwama Niger.
Sauti
9'57"