Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Waandamanaji wanapaswa kujilinda, na kuwalinda wengine dhidi ya COVID-19-WHO
Waandamanaji ambao wanataka kwenda mitaani ili kupaza sauti zao ambazo wanataka zisikike, wanatakiwa kuchukua kila tahadhari ya kutokuambukizwa virusi vya corona au kuwaambukiza wengine, katika kipindi hiki ambacho bado mlipuko huu haujakaribia mwisho wake, limesema shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO.
05 JUNE 2020
COVID-19 yakwamisha harakati za kulinda wanyamapori- WWF
Wakati dunia hii leo ikipaza sauti kuhusu utunzaji wa bayonuai ikiwemo viumbe vilivyomo duniani, nchini Tanzania harakati za kulinda wanyama walio hatarini kutoweka wakiwemo tembo na faru weusi ziko hatarini kutokana na ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 uliokumba dunia tangu mwezi Machi mwaka huu.
Vitendo vya uharibifu wa mazingira vyasababisha mazingira kutuma ujumbe - Guterres
Mazingira yanatutumia ujumbe dhahiri ya kwamba tunaharibu mazingira yetu ya asili kwa hasa yetu wenyewe, hivyo ndiyo alivyoanza Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya mazingira duniani hii leo Juni 5, maudhui yakiwa bayonuai.