Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

02 June 2020

Jaridani la Umoja wa Mataifa hii leo:

-Wahisani wa kimataifa wanakutana leo katika mkutano ulioitishwa na Ufalme wa Saudi ana Umoja wa Mataifa ili kuchangisha fedha kwa ajili hatua za kibinadamu kunusuru Maisha ya mamilioni ya watu nchini Yemen.

-Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu kwenye Umoja wa Mataifa, Michelle Bachelet ametaka hatua za dharura zichukuliwe ili kukabilia na ubaguzi katika utoaji wa huduma dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona.

Sauti
12'55"