Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 ni tishio kubwa kwa raia waliokumbwa na mizozo:UN
Raia wasio na hatia ambao wamekwama katikati ya machafuko hivi sasa wanakabiliwa na tishio jipya kutoka kwa janga la virusi vya corona au COVID-19 , Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameliambia Baraza la Usalama hii leo na kuonya kwamba janga hili janga hili linatumia fursa ya hali tete inayoikabili dunia.
Zaidi ya kijana 1 kati ya 6 hana ajira sababu ya COVID-19: ILO
Tathimini mpya iliyotolewa leo na shirika la kazi duniani ILO kuhusu athari za janga la virusi vya corona au COVID-19 imedhihirisha hali halisi ya athari mbaya na kubwa katika ajira ya vijana na pia kuelezea hatua zinazochukuliwa kuhakikisha watu wanarejea salama katika mazingira ya kazi.
27 MEI 2020
Kwenya Jarida la Umoja wa mataifa hii leo
-COVID-19 yawa upenyo wa kutangaza maziwa ya kopo badala ya maziwa ya mama
-Tutasikia kauli ya mwandishi wa habari wa kujitegemea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na jinsi COVID-19 imebadilisha maisha ya familia yake.
-Pamoja na kuleta adha COVID-19 pia imekuwa faraja kwa wengine: tutasikia kutoka kwa Fundi Beatrice kutoka Tanzania anyeshona barakoa.
Pamoja na kuleta adha COVID-19 pia imenisadia silali njaa:Fundi Beatrice
Mlipuko wa virusi vya Corona au COVID-19 kwa kiasi kikubwa umeathiri kila nyanja ya maisha ya watu duniani kote ukiacha kwamba umesababisha mamilioni ya vifo lakini pia umeathiri uchumi na maisha ya kijamii.
COVID-19 yawa upenyo wa kutangaza maziwa ya kopo badala ya maziwa ya mama- Ripoti
Ripoti mpya ya mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau, inaonesha kuwa juhudi za kukomesha matangazo ya maziwa ya kopo kwa ajili ya watoto wachanga zinaendelea kukumbwa na mkwamo hasa wakati huu wa janga la ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19.
COVID-19 imebadili maisha ya familia yangu- Mwanahabari Kanyinda
Ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, upo na chonde chonde tujikinge. Ni kauli ya mwandishi wa habari wa kujitegemea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC aliyoitoa baada ya kupona ugonjwa huo ulioenea katika mataifa 216 duniani.