Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Wakazi wa Nairobi wahaha kujinasua wakati huu wa janga la virusi vya Corona
Wakati ulimwengu bado unaendelea kutafakari ni kwa zipi utashinda vita dhidi ya virusi vya COVID-19, mamilioni ya watu wamejikuta kwenye hali ambayo hawakutarajia. Baadhi ya nchi za Afrika bado zinaendelea kushuhudia kuongeza kwa maambukizi ya virusi vya Corona. Kwa mfano nchini Kenya idadi ya wagonjwa inaongezeka kwa kasi suala ambalo limewatia hofu watu
Ulemavu alio nao mtoto huyu haukumzuia kusaka kipato kwa ajili ya familia yake
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, athari za janga la virusi vya Corona au COVID-19 zimekuwa mbayá zaidi kwa watoto wenye ulemavu, ambapo mtoto mmoja mkazi wa mji mkuu Kinshasa, ambaye ni kiziwi, amelazimika kusaka mbinu za kuweza kupata kipato ili kusaidia familia yake. John Kibego na maelezo zaidi.
Kinshasa, mji mkuu wa DR Congo katika video hii ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF yenye lengo la kuangazia sauti za vijana katikati ya janga la COVID-19, anaonekana Steve Okito, mtoto mwenye umri wa miaka 14.
Mtoto kiziwi alazimika kuosha magari jijini Kinshasa ili alee familia yake
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, athari za janga la virusi vya Corona au COVID-19 zimekuwa mbayá zaidi kwa watoto wenye ulemavu, ambapo mtoto mmoja mkazi wa mji mkuu Kinshasa, ambaye ni kiziwi, amelazimika kusaka mbinu za kuweza kupata kipato ili kusaidia familia yake.
Tanzania inavyokabili janga la corona
Ni miezi miwili na zaidi sasa tangu Tanzania itangaze mgonjwa wake wa kwanza wa virusi vya COVID-19. Tangu tarehe 16 mwezi wa tatu mwaka huu mengi yamejiri nchini Tanzania kufuatia kuzuka kwa janga la ugonjwa huo unaoathiri dunia nzima.
Serikali lazima ziwalinde wahamiaji wakati wa COVID-19
Wataalam wa haki za binadamu leo wametoa wito kwa serikali kulinda haki za wahamiaji na familia zao bila kujali hadhi zao za uhamiaji wakati na baada ya janga la virusi vya corona au COVID-19.
26 MEI 2020
Katika Jarida maalum la Habari hii leo Flora Nducha anakuletea
-Walinda amani wawili wanawake mmoja kutoka Brazili na mwingine kutoka India wameshinda tuzo ya Umoja wa Mataifa ya mwanajeshi mchagizaji wa masuala ya kijinsia kwa mwaka 2019. Wanajeshi hao Meja Suman Gawani kutoka India na kamanda Carla Monteiro Araujo kutoka Brazili watakabidhiwa tuzo hiyo Ijumaa ya 29 Meisiku ya walinda amani duniani.