Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

UNIC/Stella Vuzo

Mbinu dhidi ya virusi vya Corona zachangia uhifadhi wa mazingira- UNEP

Naam na sasa tuelekee nchini Tanzania kusikiliza sehemu ya mchango au ushiriki wa shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP katika mapambano dhidi ya virusi vya corona, COVID-19. Katika mahojiano haya yaliyofanywa na Hilda Phoya wa kituo cha habari za Umoja wa Mataifa UNIC Dar es salaam, Clara Makenya ambaye ni Mwakilishi wa UNEP nchini Tanzania anaanza kwa kueleza hatua zinazochukuliwa na shirika lake katika kupambana na COVID-19.

 

Mahojiano haya yameandaliwa na Hilda Phoya, UNIC Dar es salaam

 

 

Sauti
5'39"

25 05 2020

Katika Jarida maalum la habari hii leo Flora Nducha anakuletea

Leo ikiwa ni siku ya Afrika Umoja wa Mataifa umelisihi bara hilo na nchi zinazofanya uchaguzi kudumisha demokrasia wakiendesha uchaguzi huo hata wakati huu wa janga la virusi vya corona au COVID-19

 

Utafiti mpya uliochapishwa katika jarida la kitabibu la Lancet, umebaini kusambaa kwa ugonjwa wa saratani ya koo na sababu kuu ikiwa ni uwepo wa mashine za uchunguzi zinazofanya uchunguzi kupita kiasi hususan katika nchi za kipato cha kati.

 

Sauti
9'57"