Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Viongozi wa dunia washikamana kwa wito wa fursa ya chanjo kwa wote dhidi ya COVID-19
Zaidi ya viongozi wa kimataifa 150 leo wamezindua wito wa fursa kwa wote ya upatikanaji wa chanjo ya virusi vya corona au COVID-19 katika siku za usoni.
UNMISS yasambaza tenki za maji sokoni kudhibiti COVID-19 Juba Sudan Kusini
Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS, katika kuunga mkono juhudi za kitaifa za kudhibiti kusambaa kwa virusi vya corona au COVID-19, wamesambaza tenki za maji katika maeneo ya soko yenye msongamano wa watu mjini Juba.
14 Mei 2020
Mwakilishi wa WHO Burundi afurushwa, ofisi ya WHO kanda ya Afrika yazungumza. Huko Sudan Kusini UNMISS yaingia sokoni, kulikoni? Katibu Mkuu wa UN azindua sera ya kusaida afya ya akili wakati huu wa janga la Corona au COVID-19, na mashinani tunakwenda Ituri nchini DRC, kilio cha mama mkimbizi wa ndani na makala ni nchini Kenya. Karibu!
Afya ya akili ni msingi wa kila kitu kwenye COVID-19 - Guterres
Ugonjwa wa virusi vya Corona ukiendelea kutikisa dunia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezindua muhtasari wa mkakati wa kushughulikia afya ya akili ambayo hivi sasa inatetereka kutokana na janga la COVID-19.
Burundi yamfurusha Mkuu wa WHO siku chache kabla ya uchaguzi mkuu, WHO yazungumza
Shirika la afya la Umoja la Umoja wa Mataifa, WHO, limesema linawasiliana na serikali ya Burundi ili kufahamu sababu ya kufukuzwa kwa mwakilishi wake nchini humo pamoja na wafanyakazi wengine watatu. Serikali ya Burundi ilitangaza jana kumfukuza mwakilishi huyo Dkt. Walter Kazadi Mulombo, ikiwa ni siku chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini humo.