Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
‘Uharaka wa kuchukua hatua’ kwa ajili ya maendeleo endelevu, ni mkubwa zaidi kuliko wakati mwingine wowote wakati janga la corona likiendelea
COVID-19 ikiendelea inaendelea kuvuruga maisha na ustawi kote duniani, hii leo Jumatatu Umoja wa Mataifa umefanya mjadala mpana wa kisera kusisitiza suluhisho la ushirikiano wa kimataifa ili kupunguza janga wakati pia ulimwengu ukirejea katika mkondo wa kufikia Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu, SDGs.
COVID-19 haitambua rangi, kabila wala taifa - Shearer
Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umesema umedhamiria kulisaidia taifa hilo changa kabisa duniani kupambana na janga la corona au COVID-19 wakati huu likiwa katika harakati za kujikwamua kutoka kwenye vita vya wenyewe kwa wenye. Jason Nyakundi na maelezo zaidi.
Tusipokuwa makini, COVID-19 itatowesha mafanikio dhidi ya UKIMWI-UN
Janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 linaweza kurejesha nyuma mafanikio yaliyopatikana katika kutokomeza ugonjwa wa virusi vya Ukimwi, AIDS, yamesema mashirika ya Umoja wa Mataifa, lile la afya, WHO na lile la kukabiliana na UKIMWI, UNAIDS.
Hakuna aliye na kinga dhidi ya COVID-19 Sudan Kusini, tupambane nayo pamoja:UNMISS
Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umesema umedhamiria kulisaidia taifa hilo changa kabisa duniani kupambana na janga la corona au COVID-19 wakati huu likiwa katika harakati za kujikwamua kutoka kwenye vita vya wenyewe kwa wenye.