Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Ni wajibu wetu kuwalinda Watoto wakati huu wa COVID-19
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo ametoa wito wa kuwalinda Watoto wakati huu mlipuko wa janga la virusi vya corona au COVID-19 ukisambaa kote duniani na kushuhudiwa mwenendo unaotia hofu.
Ni vigumu kwa wananchi kuamini kuwa Ebola imeibuka tena DRC:WHO
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako wagonjwa wapya wanne wa Ebola wamebainika tangu tarehe 10 mwezi huu wa Aprili, watoa huduma wanaelezea kile ambacho wanakabiliana nacho katika kupambana na mlipuko huu wakati huu ambapo taifa hilo la Maziwa Makuu pia linakabiliwa na ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 na machafuko katika baadhi ya majimbo.
COVID-19 yazidisha ubaguzi na chuki duniani-Achiume
Mtaalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa dhidi ya masuala ya ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni , ubaguzi na hali zingine za kutovumiliana profesa Tendayi Achiume amesema wakati huu wa janga la virusi vya Corona au COVID-19 hali hizi zimedhihirika kuongezeka.
16 APRILI 2020
Miongoni wa habari ambazo Flora Nducha anakuletea katika Jarida la Umoja wa Mataifa hii leo
- Ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni na hali ya kutovumiliana vimeongezeka wakati huu wa mlipuko wa virusi vya Corona au COVID-19 kwa mujibu wa mtaalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Tendayi Achiume
-Huko Congo DRC visa vipya vya Ebola vimeripotiwa huku taifa hilo la maziwa makuu likiendelea kukabiliana na majanga mengine kama COVID-19,utapiamlo na vita limesema shirika la afya duniani WHO.
Chuki na unyanyapaa vimeongezeka wakati huu wa COVID-19:Achiume
Mtaalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa dhidi ya masuala ya ubaguzi wa rangi, chuki dhidi ya wageni , ubaguzi na hali zingine za kutovumiliana profesa Tendayi Achiume amesema wakati huu wa janga la virusi vya Corona au COVID-19 hali hizi zimedhihirika kuongezeka.
Wananchi DRC hawaamini kuwa Ebola imeibuka tena- WHO
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambako wagonjwa wapya wanne wa Ebola wamebainika tangu tarehe 10 mwezi huu wa Aprili, watoa huduma wanaelezea kile ambacho wanakabiliana nacho katika kupambana na mlipuko huu wakati huu ambapo taifa hilo la Maziwa Makuu pia linakabiliwa na ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 na machafuko katika baadhi ya majimbo