Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Huu si wakati wa kusitisha ufadhili kwa WHO- Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema huu si wakati wa kupunguza rasilimali za kufanikisha operesheni za shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO ambalo linakabiliana na janga la virusi vya Corona au COVID-19.
Umuhimu wa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa katika wakati huu wa janga la Corona
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa limechukua jukumu muhimu katika kukabiliana na janga la COVID-19, tangu mgonjwa wa kwanza alipotangazwa katika mji wa China, Wuhan mnamo mwezi Desemba mwaka jana 2019. Kwenye mkutano na waandishi wa habari mkuu wa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus, anazitaja sababu tano za umuhimu wa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa katika wakati huu wa Janga la Corona kuwa ni:
Chuki na taarifa potofu vyatawala zama hizi za COVID-19:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wakati dunia ikipambana na janga la mlipuko wa COVIDI-19, changamoto kubwa kabisa kuwahi kuikabili dunia tangu vita vya pili vya dunia, kunashuhudiwa pia mlipuko mwingine wa hatari, ambao ni mlipuko wa taarifa potofu
Uganda yakaza uzi wa mikakati ya kudhibiti COVIDI-19
Nchini Uganda, Raisi Yoweri Kaguta Museveni ametangaza kurefusha muda wa kutekeleza sheria ya kutotembea usiku, kubana mijumwiko, usafiri wa umma na ule wa magari binafsi kwa wiki tatu katika juhudi za kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona au COVID-19.
14 APRILI 2020
Katika Jarida la Habari za Umoja wa Maaifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Uganda yaongeza muda wa wiki tatu kutekeleza sheria za kupambana na virusi vya Corona au COVIDI-19 ikiwemo marufuku ya kutembea usiku, kutumia usafiri wa umma na magari binafsi.
-Watoto milioni 117 kote duniano wako katika hatari ya kukosa chanjo ya surua ya kuokoa maisha kutokana na mlipuko wa COVIDI-19 yameonya mashirika ya Umoja wa Mataifa ya UNICEF na WHO
Tulichojifunza kuhusu Ebola chaweza kusaidia vita dhidi ya COVID-19:Dkt. Moeti
Juhudi kubwa zikiendelea kote duniani kupambana na mlipuko wa virusi vya Corona au COVID 19, barani Afrika idadi ya wagonjwa inaendelea kuongezeka na Kwa mujibu wa mkurugenzi wa shirika la afya duniani WHO kanda ya Afrika Dkt. Matshidiso Moeti.
Uganda yarefusha muda wa amri ya kutotembea usiku, COVID-19
Nchini Uganda, Raisi Yoweri Kaguta Museveni ametangaza kurefusha muda wa kutekeleza sheria ya kutotembea usiku, kubana mijumwiko, usafiri wa umma na ule wa magari binafsi kwa wiki tatu katika juhudi za kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona au COVID-19.
Ndege ya kwanza ya UN iliyosheheni msaada wa COVID-19 kuondoka leo kuelekea nchi za Afrika:WHO/WFP/AU
Ndege ya kwanza ya mshikamano ya Umoja wa Mataifa inatarajiwa kuondoka leo mjini Addis Ababa Ethiopia kuelekea nchi mbalimbali za Afrika ikiwa imesheheni msaada na vifaa ya kukabiliana na mlipuko wa virusi vya Corona au COVID-19.
Kutokana na ongezeko la COVID-19, zaidi ya watoto milioni 117 wako hatarini kukosa chanjo ya surua
Kutokana na taarifa iliyotolewa hii leo mjini Atlanta na New York Marekani, pamoja na Geneva Uswisi, wakati COVID-19 ikizidi kusambaa duniani, zaidi ya watoto milioni 117 katika nchi 37 wanaweza kukosa kupokea chanjo ya kuokoa maisha dhidi ya surua.