Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Picha ya maktaba ikionesha WHO na wadau wengine walipopeleka msaada wa kudhibiti ugonjwa wa surua katika eneo la West Darful mwezi April 2015 nchini Sudan. Huduma kama hiyo sasa iko katika majimbo ya Sudan Kusini
WHO Sudan

Umuhimu wa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa katika wakati huu wa janga la Corona

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa  limechukua jukumu muhimu katika kukabiliana na janga la COVID-19, tangu mgonjwa wa kwanza alipotangazwa katika mji wa China,  Wuhan mnamo mwezi Desemba mwaka jana 2019. Kwenye mkutano na waandishi wa habari  mkuu wa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus, anazitaja sababu tano za umuhimu wa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa  katika wakati huu wa Janga la Corona kuwa ni: 

14 APRILI 2020

Katika Jarida la Habari za Umoja wa Maaifa hii leo Flora Nducha anakuletea

-Uganda yaongeza muda wa wiki tatu kutekeleza sheria za kupambana na virusi vya Corona au COVIDI-19 ikiwemo marufuku ya kutembea usiku, kutumia usafiri wa umma na magari binafsi.

-Watoto milioni 117 kote duniano wako katika hatari ya kukosa chanjo ya surua ya kuokoa maisha kutokana na mlipuko wa COVIDI-19 yameonya mashirika ya Umoja wa Mataifa ya UNICEF na WHO

Sauti
14'1"