Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Mwanamke akiwa amembeba binti yake katika kituo cha Wisdom kilichopo eneo la Gurei mjini Juba nchini Sudan kusini baada ya kupigwa na mumewe.
© UNICEF/Albert Gonzalez Farran

Ukatili majumbani ukiongezeka, Katibu Mkuu wa UN ataka sitisho la vitendo hivyo

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa hatua za kukomesha ghasia na ukatili majumbani dhidi ya wanawake na wasichana, kufuatia ripoti kuwa vitendo hivyo vimeshamiri hivi sasa maeneo mbali mbali duniani baada ya serikali kutaka wananchi wasalie majumbani kuepusha kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19.

Sauti
2'9"