Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Baraza Kuu lapitisha azimio la mshikamano duniani kutokomeza virusi vya Corona
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limepitisha azimio la kuonesha mshikamano ya vita dhidi ya virusi vya Corona au COVID-19.
Vita dhidi ya virusi vya Corona, COVIDI 19 ni jukumu la kila mtu:UN
Kufuatia kusambaa kwa mlipuko wa virusi vya Corona COVID-19 sehemu mbalimbali duniani Umoja wa Mataifa na mashirika yake umekuwa ukihimiza kila mtu kuchukua hatua ili kuhakikisha ugonjwa huu hatari ambao umeshakatili maisha ya maelfu ya watu na kuathiri malaki ya wengine hausambai zaidi.
Kufuatia mlipuko wa COVID-19 mkutano wa COP26 waahirishwa:UN
Umoja wa Mataifa umetangaza kuahirishwa kwa mkutano wa 26 wa kimataifa wa mbadiliko ya tabianchi COP26 uliokuwa ufanyike baadaye mwaka huu kutokana na janga la kimataifa la virusi vya Corona , COVID-19.
Kambini Zaatar Jordan maandalizi dhidi ya COVID-19 yashika kasi:UNHCR
UNHCR imesema inafanya kazi na wizara ya afya ya Jordan kuandaa mazingira ya kupambana na virusi vya corona.
Iyad Shyauiat, ambaye ni Afisa afya katika UNHCR anasema, “tunawapa mwongozo kuhusu taratibu wanazozifanya ndani ya kiliniki zao kwa maana ya kudhibiti maambukizi na kujiandaa na utayari.”
UNHCR imesema hadi sasa hakuna mgonjwa yeyote wa COVID-19 ambaye ameshapatikana miongoni mwa wakimbizi ndani ya kambi lakini hospitali ndani ya kambi ambayo inawahudumia wakimbizi wa Syria takribani 76,000, inajiandaa kwa mlipuko wa ugonjwa huo.
UNMISS yashirikiana na Sudan Kusini kujiandaa kwa ajili ya COVID-19
Soko la kila wiki huko Sakure, karibu na mpaka kati ya Sudani Kusini na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC limefungwa kama sehemu ya juhudi za Serikali ya Sudani Kusini kudhibiti tishio la kimataifa la virusi vya corona au COVID-19
Soko hilo lilikuwa na shuhguli nyingi kila Ijumaa huku wafanyabiashara kutoka nchi zote mbili wanakutana na kubadilishana bidhaa, lakini, serikali ya Sudani Kusini hivi karibuni imetangaza kufungwa kwa mipaka yake na nchi jirani. Na hatua hiyo imesababisha soko kufungwa pia.
02 APRILI 2020
Katika Jarida la habari hii leo assumpta Massoi anakuletea
-Siku ya uelimishaji kuhusu usonji ikiadhimishwa leo Umoja wa Mataifa umetoa wito kuhakikisha watu hao wanajumuisha katika harakati za kupambana na janga la virusi vya Corona , COVID-19
-Huko nchini Suda Kusini japo bado hakuna mgonjwa yeyote wa virusi vya Corona COVID-19 mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS kwa kushirikiana na serikali wachukua hatua kujikinga ikiwa ni pamoja na kufunga soko kubwa mpkani wa nchi hiyo na DRC
Janga la COVID-19 linawaweka watu wenye usonji katika hatari kubwa.
Kupitia ujumbe wake maalum kwa siku hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema siku ya uelimishaji kuhusu usonji inaadhimishwa kwa kutambua na kusherehekea haki za watu wenye usoni na kwamba “Mwaka huu siku hii inaadhimishwa katikati ya janga la kimataifa la kiafya ambalo hatujawahi kulishuhudia katika maisha yetu, janga ambalo linawaweka watu wenye usonji katika hatari kubwa kutokana na virusi vya Corona na athari zake katika jamii.”
Hofu ya maambukizi ya COVID-19 yasababisha soko la Sakure kufungwa nchini Sudan Kusini
Soko la kila wiki huko Sakure, karibu na mpaka kati ya Sudani Kusini na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC limefungwa kama sehemu ya juhudi za Serikali ya Sudani Kusini kudhibiti tishio la kimataifa la virusi vya corona au COVID-19
Hakuna COVID-19 katika kambi ya Zaatar lakini tumeanza kujipanga-UNHCR
UNHCR imesema inafanya kazi na wizara ya afya ya Jordan kuandaa mazingira ya kupambana na virusi vya corona.
COVID-19 ikitikisa, mlo uwe vipi?
Wakati wazazi wengi wanatafuta milo iliyokwishapikwa tayari na vyakula vya kusindikwa kama njia ya haraka na ya bei nafuu ya kulisha familia, kuna njia mbadala rahisi, za bei nafuu na zenye afya hasa wakati huu wa ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19.