Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Tijjani Muhammad-Bande ashiriki mkutano kwa njia ya mtandao wa wanachama wa UN kuhusu virusi vya corona.
United Nations/Reem Abaza

UN yawajulisha nchi wanachama kuhusu mapambano dhidi ya COVID-19

Katika mkutano maalum kupitia njia ya mtandao uliofanyika leo Katibu Mkuu wa moja wa Mataifa, Rais wa Baraza Kuu la Umoja huo, Baraza la Usalama na baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC wamezijulisha nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuhusu juhudi za Umoja huo katika kupambana na virusi vipya vya Corona, COVID-19 na kuendelea na kazi muhimu ya shirika hilo duniani kote.

WFP/Challiss McDonough

Mlipuko wa COVID-19 unaathiri uwasilishaji wa mlo shuleni-WFP

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP leo limezindua ramani mpya ya kidijitali inayodhihirisha athari za virusi vya Corona, COVID-19 katika program zake za mlo mashuleni. Flora Nduicha na taarifa kamili

(TAARIFA YA FLORA NDUCHA)

Kwa mujibu wa WFP ramani hiyo ambayo ni ya “ufuatiliaji wa kimataifa wa mlo mashuleni wakati wa kufungwa shule kutokana na mlipuko wa COVID-19 inatoa inatoa maenedeleo mapya ya kila siku kuhusu kufungwa kwa shule na idadi ya Watoto ambao hawapati tena mlo mashuleni kutokana na janga hili la Corona.

Sauti
1'15"
© Julius Mwelu/ UN-Habitat

Mapambano dhidi ya COVID-19 Kenya

Watu waliopoteza maisha hadi sasa kote duniani kutokana na virusi vya corona ikiwa imevuka 20,000 huku zaidi ya watu nusu milioni kote duniani wakiambukizwa virusi hivyo hatari nchini Kenya kama zilivyo nchi nyingine, mapambano dhidi ya ugonjwa huo yanaendelea. Katika makala ya leo, mwandishi wetu wa Nairobi Jason Nyakundi anaangazia tahadhari ambazo watu wa Kenya wanazichukua kujikinga na virusi vya corona na changamoto wanazokumbana nazo.

Sauti
6'6"