Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
UNICEF kuongeza msaada katika nchi 145 ili kuwezesha watoto kuendelea kujifunza, wakati huu wa COVID-19
Kufungwa kwa shule katika mataifa mbalimbali kukiingilia utaratibu wa masomo kwa zaidi ya asilimia 80 ya wanafunzi duniani kote, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limetangaza hii leo kuwa litaongeza msaada wake kwa nchi zote ili kuwasaidia watoto kuendelea na ujifunzaji.
Mkutano wa G-20 UN yasisitiza mshikamano kukabili COVID-19
Katika mkutano huo ambao ulijikita na COVID-19 Guterres ametoa wito akisistiza kwamba “Hatua za pamoja za kimataifa zinahitajika ili kuweza kushinda vita dhidi ya virusi vya Corona na pia mshikamano na wale wasiojiweza ni muhimu.”
Pande kinzani Sudan wekeni silaha chini tokomezeni COVID-19
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika, AU, huko Darfur, Sudan, Jeremiah Mamabolo amekazia kauli ya Katibu Mkuu wa umoja huo ya kutaka sitisho la mapigano kwenye maeneo ya mizozo wakati huu ambapo virusi vya Corona, COVID-19, vimeshasambaa katika mataifa 194.
Elimu kwa jamii kuhusu kuzuia kuenea kwa virusi vya corona Tanzania
Wakati ulimwengu unaendelea na mapambano dhidi ya virusi vya corona, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linaeleza wasiwasi wake kuhusu elimu ya watoto kutokana na ulazima wa kufungwa kwas hule katika mataifa takribani 120 hivi sasa duniani kote. Shirika hilo linasema zaidi ya nusu ya wanafunzi wote ulimwenguni wameathiriwa na hatua ya kufungwa kwa shule ikiwa ni sehemu ya juhudi za kutokomeza ugonjwa huo.
Pamoja na kupambana na COVIDI-19 tusisahau chanjo:UNICEF
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesihi serikali duniani kote kuanza mipango thabiti ya utoaji chanjo kwa watoto pindi janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 litakapodhibitiwa.
Zanzibar yachukua hatua kukabili COVID-19
Katika kuepusha kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19 huko visiwani Zanzibar nchini Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imechukua hatua katika sekta ya mahakama ikiwemo kusitisha kwa muda usikilizaji wa kesi za madai na jinai.
COVID-19 isiwe chanzo cha kusahau huduma muhimu za chanjo kwa watoto- UNICEF
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesihi serikali duniani kote kuanza mipango thabiti ya utoaji chanjo kwa watoto pindi janga la ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 litakapodhibitiwa.
COVID-19: Zanzibar yachukua hatua kupunguza mlundikano magerezani
Idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona, huko visiwani Zanzibar nchini Tanzania ikiwa imefikia wagonjwa wawili, hii leo serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetangaza hatua za kuhakikisha sekta ya mahakama inaunga mkono hatua za kudhibiti kuenea kwa virusi vya Corona, COVID-19 ikiwemo kusitisha kwa muda usikilizaji wa kesi za madai na jinai. Omar Abdalla wa Televisheni washirika ZenjFM kutoka Zanzibar ametuandalia taarifa hii.