Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

UN News/ John Kibego

Hisia za wakimbizi nchini Uganda kufuatia mlipuko wa Corona unaoshuhudiwa duniani kote

Katika makala ya wiki hii tutakuwa nchini Uganda tukiangazia shaka na shuku miongoni mwa wakimbizi na hatua za Umoja wa Mataifa wakati huu wa maambukizi ya Corona.  

Mwandishi wetu wa Uganda, John Kibego alikwenda kambi ya wakimbizi ya Kyangwali kusikiliza shaka na shuku zao kuhusu hofu ya kuingia kwa virusi vya corona kwenye taifa hilo ambalo bado halina mgonjwa hadi leo Ijumaa. 

Sauti
4'56"