Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

18 Machi 2020

Assumpta Massoi : Hujambo na Karibu kusikiliza Jarida kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, kutoka hapa New York Marekani.

JINGLE (04”)      

ASSUMPTA:Ni Jumatano ya  Machi kumi na nane mwaka 2020, mwenyeji wako studioni hii leo ni mimi ASSUMPTA MASSOI 

Sauti
12'21"
©UNICEF/Leonardo Fernandez

Wagonjwa wa COVID-19 wafikia watatu Tanzania, mgonjwa wa kwanza afunguka

Nchini Tanzania idadi ya wagonjwa wa Corona au COVID-19 imefikia 3 baada ya wagonjwa wapya wawili kuthibitishwa hii leo wakiwa ni raia wa Marekani na Ujerumani. Taarifa zaidi na Flora Nducha.
 (Taarifa ya Flora Nducha)
 Taarifa za kuthitbishwa kwa wagonjwa hao wapya zimetolewa leo mjini Arusha nchini Tanzania na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu.
 (Sauti ya Ummy Mwalimu)

Sauti
2'45"