Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Chonde chonde wahisani tunawategemea sasa kuliko wakati mwingine wowote:UNICEF
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF ametoa rai kwa wahisani kuendelea kunyoosha mkono hasa wakati huu dunia ikikabiliana na janga kubwa la virusi vya Corona au COVID-19.
Tumeanza rasmi chanjo ya majaribio ya dhidi ya COVID-19: WHO
Shirika la afya ulimwenguni WHO leo limesema siku 60 baada ya sampuli za virusi vya Corona au COVID-19 kuwasilishwa kwa shirika hilo na Cina, chanjo ya kwanza ya majaribio imeanza.
18 Machi 2020
Assumpta Massoi : Hujambo na Karibu kusikiliza Jarida kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, kutoka hapa New York Marekani.
JINGLE (04”)
ASSUMPTA:Ni Jumatano ya Machi kumi na nane mwaka 2020, mwenyeji wako studioni hii leo ni mimi ASSUMPTA MASSOI
Wagonjwa wa COVID-19 wafikia watatu Tanzania, mgonjwa wa kwanza afunguka
Nchini Tanzania idadi ya wagonjwa wa Corona au COVID-19 imefikia 3 baada ya wagonjwa wapya wawili kuthibitishwa hii leo wakiwa ni raia wa Marekani na Ujerumani. Taarifa zaidi na Flora Nducha.
(Taarifa ya Flora Nducha)
Taarifa za kuthitbishwa kwa wagonjwa hao wapya zimetolewa leo mjini Arusha nchini Tanzania na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu.
(Sauti ya Ummy Mwalimu)
Tukisalia nyumbani kujikinga na COVID-19, tusiwasahau wasio na makazi:UN
Wakati huu ambapo serikali zikitegemea watu kusalia nyumbani ili kusaidia kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya Corona, COVID-19, ni lazima nchi zichukue hatua za kuzuia mtu yeyote kukosa makazi na kuhakikisha fursa ya mahali pa kukaa kwa wale wasio na makazi.
COVID-19 Tanzania : Wagonjwa wafikia 3, Vyuo Vikuu vyafungwa, mgonjwa wa kwanza azungumza.
Nchini Tanzania idadi ya wagonjwa wa Corona au COVID-19 imefikia 3 baada ya wagonjwa wapya wawili kuthibitishwa hii leo wakiwa ni raia wa Marekani na Ujerumani.
Pamoja na COVID-19 mamilioni bado wahitaji misaada- OCHA
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya misaada ya dharura, OCHA imekumbusha kuwa mamilioni ya watu walio hatarini bado wanategemea misaada ya kuokoa maisha inayotolewa na Umoja wa Mataifa.