Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
Nchi za Afrika zizalishazo mafuta kupoteza dola bilioni 65 kutoka na virusi vya Corona
Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya uchumi barani Afrika, UNECA, imeonya kuwa janga la virusi vya Corona lililokumba dunia hivi sasa litasababisha nchi za Afrika zinazozalisha mafuta kupoteza dola bilioni 65.
COVID-19: Sasa ni wakati wa busara si kupagawa na sayansi na si unyanyapaa - Guterres
Shaka na shuku zikiendelea kugonga vichwa vya wakazi wa dunia hii wakati huu wa kusambaa kwa virusi vya Corona, au COVID-19, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema huu ni wakati wa busara na sio kupagawa, wakati wa sayansi na sio unyanyapaa na zaidi ya yote ni wakati wa ukweli na si hofu.
Baada ya mgonjwa wa Corona kuthibitishwa Kenya, mikusanyiko mikubwa yapigwa marufuku
Nchini Kenya kufuatia kuthibitishwa kwa mgonjwa wa kwanza wa virusi vya Corona, COVID-19, shirika la afya ulimwenguni WHO nchini humo limesema linashirikiana na serikali katika hatua zote za kudhibiti kusambaa kwa virusi hivyo katika taifa hilo la Afrika Mashariki, wakati huu ambapo mgonjwa huyo amewekwa katika karantini kwenye hospitali ya Kenyatta jijini Nairobi hadi pale atakapobainika kuwa hana tena virusi.
WHO yaunda mfuko kukabili COVID-19; Ulaya sasa ndio kitovu kipya cha virusi hivyo hatari
Ulaya sasa ndio kitovu kipya cha zahma ya mlipuko wa virusi vya Corona, amesema leo Ijumaa mkurugenzi mkuu wa shirika la afya ulimwenguni WHO Dkt. Tedros Adhamon Ghebreyesus.
Mgonjwa wa Corona nchini Kenya alirejea nyumbani kutokea Marekani akipitia Uingereza
Nchini Kenya kufuatia kuthibitishwa kwa mgonjwa wa kwanza wa virusi vya Corona, COVID-19, shirika la afya ulimwenguni WHO nchini humo limesema linashirikiana na serikali katika hatua zote za kudhibiti kusambaa kwa virusi hivyo katika taifa hilo la Afrika Mashariki, wakati huu ambapo mgonjwa huyo amewekwa katika karantini kwenye hospitali ya Kenyatta jijini Nairobi hadi pale atakapobainika kuwa hana tena virusi.
13 Machi 2020
Nchini Kenya kufuatia kuthibitishwa kwa mgonjwa wa kwanza wa virusi vya Corona, COVID-19, shirika la afya ulimwenguni WHO nchini humo limesema linashirikiana na serikali katika hatua zote za kudhibiti kusambaa kwa virusi hivyo katika taifa hilo la Afrika Mashariki. Aibu ya kurejea nyumbani mikono mitupu inatuponza, wasema wahamiaji. Programu ya kuimarisha stadi yasaidia mkimbizi kutoka Colombia kufikia ndoto zake.
UN yaendelea kuchukua hatua zaidi dhidi ya COVID-19
Katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani hatua zinaendelea kuchukuliwa kukabiliana na mlipuko wa virusi vya Corona, COVID-19 unaoitikisa dunia hivi sasa.