Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Hapa ni nchini China, mhudumu akiacha kifurushi nje ya nyumba kwa kuwa hawaruhusiwi kuingia kwenye majengo kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona nchini humo.
Man Yi

UN yatoa dola milioni 15 za kimarekani kukabiliana na COVID-19

Umoja wa Mataifa kupitia ofisi yake ya kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura OCHA umetoa dola milioni 15 za kimarekani kutoka katika mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa CERF ili zisaidie juhudi za ulimwengu kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa wa COVID-19, hususani katika nchi zenye mfumo duni wa huduma za afya.