Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

Watu wakiwa wamevaa vifaa vya kinga kwenye duka mji wa mashariki mwa China, Nanjing.
UN News/Li Zhang

Dunia inapungukiwa vifaa vya kujikinga wakati idadi ya waathirika wa corona ikipanda-WHO

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya ulimwenguni WHO, Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus ameonya kuwa ulimwengu unakabiliwa na sintofahamu kubwa katika soko la vifaa vya kujikinga na kutoa wito kwa nchi na makampuni kufanya kazi na WHO "kuhakikisha matumizi sawa ya vifaa na kuzingatia mizania katika soko" katika kukabiliana na virusi vipya vya corona (2019-nCoV).