Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Rahot akiwa na mjukuu wake, Hassan, kijijini ambako alihamia karibu na kituo cha lishe kinachoendeshwa na SCI na kufadhiliwa na SHF.
Sara Awad – Save the Children

Napanda milima kuhakikisha mjukuu wangu anapata tiba ya Utapiamlo

Kila siku asubuhi na mapema kukipambazuka na jua kuchomoza Rahot mwenye umri wa miaka 55 huamka na kumbeba mgongoni mjukuu wake Hassan tayari kwakuaza safari ya takriban kilometa 20 yenye vilima kwenda kituo cha kumpatia lishe mjukuu huyo ili kuokoa maisha yake kutokana na kuwa na utapiamlo mkali.