Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

© UNICEF/Karel Prinsloo

Mabadiliko ya tabianchi yawaathiri wafugaji Arusha Tanzania

Umoja wa Mataifa ukiendelea kutaka hatua zaidi kwa ajili ya tabianchi kama njia mojawapo ya kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya tabianchi nchini Tanzania madhara hayo yako dhahiri kwa wafugaji wa wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha ambao kupitia taarifa hii iliyoandaliwa na Mathias Tooko wa Radio washirika Loliondo FM wanaeleza hali ilivyokuwa zamani na sasa.
(Taarifa ya Mathias Tooko)

Sauti
1'54"

30 DESEMBA 2021

Katika Jarida la habari hii leo Assumpta Massoi anakuletea

-Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini Kenya limechukua hatua ya kushirikiana na viongozi wa dini ikiwemo wale wa madhehebu ya kiislamu ili kusaidia kuelimisha waumini wao juu ya chanjo ya COVID-19 na faida zake katika kuepusha maambukizi

-Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na masuala ya afya ya uzani UNFPA limezindua kampeni ya Hakimiliki ya mwili kwa lengo la kukabiliana na ukatili wa kijinsia mtandaoni hususan dhidi ya wanawake na wasichana 

Sauti
12'6"