Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

FAO/Rudolf Hahn

Uhusiano kati ya biashara yetu na mazingira ni wa ajabu sana-Wauza miche ya miti Tanzania

Biashara ya uuzaji wa miche ya miti nchini Tanzania hususani katika jiji la Dar es Salaam ni ya miaka mingi. Wauzaji wanasema ingawa uhusiano kati ya miti na mazingira ni  wa wazi mno, lakini kwao uhusiano huu ni wa ajabu. Wauza miti wanasema wanauza miti ili iende kuyatunza mazingira, na mazingira kwa haraka yanawalipa kwa kuwaletea mvua ambayo ni muhimu sana kwa biashara yao. Ungana na Ahimidiwe Olotu wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam aliyefunga safari hadi katika eneo la Mabibo, Ubungo Dar es Salaam kukutana na wafanyabiashara hawa. 

Sauti
3'30"