Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mfanyakazi wa UNMAS akichunguza mabomu ya kutegwa ardhini, jimbo la Equatoria kati, Sudan Kusini.
© UN Photo/Isaac Billy

Mtu 1 huuawa kila saa kwa bomu au kilipuzi - UN

Mabomu, vilipuzi na vifaa vingine vya mlipuko vinaendelea kuua na kujeruhi watu katika maeneo mengi yenye changamoto kubwa za migogoro duniani na matokeo yake vifaa hivyo vya mlipuko, kwa wastani hukatili Maisha ya mtu mmoja kila saa, na waathirika wakubwa wakiwa ni watoto kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.

Kenya kuunda viashirio vipya vya kupima usawa wa kijinsia katika sekta ya biashara.
UNCTAD

UNCTAD/UNECA: Kenya kuunda viashirio vipya vya kupima usawa wa kijinsia katika sekta ya biashara.

Umoja wa Mataifa umekuwa ukipigia upatu lengo namba tano la Malengo Endelevu ya Umoja huo linalohimiza usawa kwa wote katika nyanja zote ifikapo mwaka 2030. Hata hivyo ili kuelewa jinsi biashara inavyoathiri wanaume na wanawake ni muhimu kuunda sera za biashara zinazojumuisha zaidi na zenye usawa ambazo zinakuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa kiuchumi kwa wote,hii inahitaji takwimu nzuri za kitaifa kuhusu jinsia katika biashara.

Audio Duration
3'8"
Hapa ni Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Brazil wanaohudumu kikosi cha kujibu mashambulizi FIB cha MONUSCO wakipatia mafunzo wanajeshi 30 kutoka jeshi la serikali, FARDC j…
MONUSCO/Ado Abdou

DRC: MONUSCO yapatia wanajeshi 30 wa FARDC mbinu za kukabili waasi msituni

Siku zikizidi kuhesabiwa kwa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, MONUSCO, kuondoka nchini humo, ujumbe huo unaendelea kutekeleza wajibu wake wa kujengea uwezo jeshi la serikali, FARDC kuweza kukabili vikundi vilivyojihami ambavyo vinatajwa kuhusika na asilimia 65 ya matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo mwezi Februari mwaka huu, kwa mujibu wa ripoti ya pamoja ya Umoja wa Mataifa na serikali. 

Sauti
2'12"